Uliiona hii? ‘msanii wa bongo Movie asema anatamani Ney wa Mitego awe mumewe wa ndoa

Afsa

Ingawa Ney wa mitego ni jina ambalo wengi tunaamini kabisa halikubaliki kwa baadhi ya  wasanii wa bongo movie hasa wasichana baada ya kutoa wimbo wake ‘Nasema Nao’, na kufikia hatua ya kurushiwa maneno makali na baadhi ya waigizaji wa kike TZ, Afsa Omary Neema 20%  yeye sio tu kuwa anamzimia Ney wa mitego, lakini anataka awe mmewe wa ndoa kabisa and that’s that.
Kwa mujibu wa blog ya wajanja club katikati ya mwezi huu, Afsa Omary a.k.a Neema 20% kwa kinywa chake alifunguka, “Si siri nampenda sana Ney wa Mitego na natamani awe mume wangu wa ndoa hata kesho kama akikubali, kama ingekuwa wasichana tunaruhusiwa kuwatongoza wanaume na kuolewa nao basi mimi ningekuwa wa kwanza kwa Ney, ana mvuto na shababi.”
Sifa hazikuishia hapo, Afsa Omary a.k.a Neema 20 alidai kuwa anampenda mwanaume anaejiamini na mtanashati na muonekano anaouona kwa Ney wa Mitego na sio mtu mwingine na atafanya kila juhudi aweze kuishi na msanii huyo ambae kila akitoa wimbo lazima ulete gumzo.
Afsa Omary, Neema 20% kama wanavyomuita ni muigizaji aliyeibuka kupitia filamu ‘Furaha Iko wapi’ iliyotungwa na msanii wa bongo fleva Hamisi Kinzasa a.k.a 20 percent.
Habari ndiyo hiyo, ukweli anao mwanadada huyu mwenyewe kwa sababu hisia za mtu hazionekani tungepima tuhakikishe. 

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates